Sunday, January 23, 2011

BERBATOV,VAN PERSIE WAPIGA 'HAT TRICK' ENGLAND

 Dimitar Berbatov

 Robin van Persie akishangilia
Washambiliaji Dimitar Berbatov wa Manchester united na Robin van Persie wa Arsenal jana walizibeba timu zao baada ya kupiga mabao matatu kila mmoja katika michezo yao ya ligi kuu ya Uingeleza maarufu kama 'Barclays premier league'

Berbatov alitupia mabao wakati man u ilipoibamiza Birmingham 5-0 huku Van persie akiisaidia Arsenal kuiangamiza Wigan Athletic mabao 3-0 mabao ya van persie aliyafunga katika dakika za 21,58 na 85.mabao mengine ya man yalitupiwa kimiani na Luis nani na mkongwe Ryan Giggs.

Kwa matokeo hayo sasa manchester united imezidi kujikita kileleni kwa kufikisha jumla ya ponti 48 huku Arsenal wakijisogeza mpaka nafasi ya pili kwa kufikisha pointi 46.




 Robin van persie akishangilia bao la tatu alilofunga dhidi ya Wigan jana.


 Wachezaji wa Manchester wakimpongeza Berbatov baada ya kufunga dhidi ya Birmingham jana.
 Matokeo mengine ya ligi hiyo ni:
Newcastle 1-Spurs 1
Fulham 2 Stoke 0
Liverpool 3 Wolves 0
Everton 2 Westham 2
Blackpool 1 Sunderland 2